Warning: Undefined array key 1 in /home/acaproso/public_html/._System/._Template/.Main.php on line 116
Ufahamu questions

Ufahamu questions | form four Kiswahili

Find Ufahamu examination questions, form four Kiswahili in acaproso.com

# Question
1

Soma kwa makini kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali yanayofuata:
Mtu hutembea njiani akajikwaa, ukucha ukang’oka au pengine hata kubwagwa chini vibaya na kisiki, kisha mtu huyu hugeuka na akakiangalia kisiki hicho, ambacho pengine huwa hata hakitazamiki.
Kama kisiki kimkwazavyo mtu atembeaye, pia mikasa mbalimbali, midogo kwa mikubwa,
huwakwaza na pengine hata kuwabwaga chini binadamu katika maisha yao. Jinsi baadhi ya mikasa hii ilivyo adhimu, mtu anapokumbuka huweza kulia. Kwa upande mwingine mtu hujionea fahari alivyopambana na mikasa hiyo kwa ujasiri hadi akaishinda au kuikwepa. Tukio kama hili hufanya shajara la mambo bora ya kukumbukwa maishani.
Maisha ya shule ni mazuri, lakini mara nyingi huwa magumu na hasa lile wingu jeusi la mitihani likaribiapo. Wanafunzi hupuuza sheria kama vile kwenda madarasani, michezoni na pengine hata kula, wakajibanza mahali pa faragha wakajisomea. Nyakati zipendwazo ni usiku wa manane, kwa kujua kuwa kila mtu amelala na kuwa hayupo mwalimu wa zamu awezayo kuzuru shule wakati huo.
Wanafunzi wenye bahati hunufaika sana kwa mpango huo wala hawagunduliwi. Wengine mara hugunduliwa wakapewa adhabu ambayo huridhika kuifanya kwani n zi kufa kwenye kidonda si hasara .
Siku hiyo ilikuwa Jumapili, nami nikajiunga katika ngoma ya kusoma na wenzangu wanne, wawili wao walikuwa viranja wa madarasa. Ilipata saa nane za usiku nasi tukaingia katika chumba cha kuoneshea picha, tukafunga mlango kwa funguo na komeo. Baada ya kuhakikisha kuwa hapana hata mwonzi mdogo wa taa uliotambaa nje, tulitoa ala zetu, kila mtu akashughulika na hamsini zake.
Hapakupita saa moja, mara tunasikia mlango unabishwa hodi, “fungua mlango! tokeni sasa hivi.” Sauti hiyo ilikuwa ya mmoja wa wanafunzi wa shule yetu. Mwanafunzi huyu aliandamana na mtu ambaye tulimtambua kwa sauti kuwa alikuwa Tatu, dada mkuu wa shule. Mioyo ilianza kutudunda kwa hofu, damu zetu zikawa karibu kuganda. Mara nilipata fahamu nikazima taa, lakini kwa bahati mbaya chumba hicho hakikuwa na madirisha ambayo kwayo tungeliweza kutoka. Kumbe mwanafunzi huyo naye alipata maarifa, alipanga viti kimoja juu ya kingine, akapanda juu na kuchungulia ndani katika mwanya uliokuwa karibu na dari. Kumulika ndani akamtambua Dora.
Dora! Dora! fungueni mlango na tokeni sasa hivi!” akang’aka, lakini tukapiga kimya humo ndani.
Mwanafunzi huyo alipoona ameshindwa kututoa, alifanya hila ya kumwita mwalimu mkuu. Naam, sauti ya simba huweza kumdondosha chini panya aliyejificha darini. “Dora fungua mlango sasa hivi!” alinguruma, sote tulibaki tumeduwaa. Dora akafungua mlango, “u shikwapo shikamana” wahenga walisema, mlango ulipofunguliwa mimi nilibana nyuma yake bila mtu kufahamu. Mwalimu mkuu aliwasha taa akachungulia ndani. Kuona hakuna mtu alizima taa akaondoka zake kwenda kuwadadisi wenzangu. Moyo ulishuka pwaa! nikatoka huku nagwaya mwili mzima, nikakimbia kwa mashaka makubwa hadi benini kwangu. Kwa vyovyote vile nilijua nilikuwa ndani.Hazikupita hata datika tano tokea nijitupe kitandani nikashtukia taa zinawashwa mabwenini. Kumbe mwalimu mkuu, mwalimu wa zamu na Tatu, wakisaidiana na akina dada kadhaa walikata shari wafanye uchunguzi wa shule nzima, ili kuona iwapo wanafunzi wote walikuwepo. Ama kweli “s iku za mwizi arobaini,” wanafunzi wapatao kumi na watano walikuwa mjini ambako kulipigwa muziki
na bendi mashuhuri kutoka Dar es Salaam. Asubuhi niliamka kichwa kizito nikauhisi mwili sio wangu. Masomo kuanza tu likapitishwa tangazo likiwaita wale wenzangu niliokuwa nao usiku na wale waliotoroka. Ilipofika saa nne, tukakuta wote wanafunga virago, nikaanza kuwa na matumaini kuwa ama kweli niliponea chupuchupu.

Maswali
(a) Fafanua maana za misemo ifuatayo kama ilivyotumika katika habari uliyosoma:
(i) Nzi kufa kwenye kidonda si hasara.
(ii) Kila mtu akashughulika na hamsini zake.
(iii) Ushikwapo shikamana.
(iv) Siku za mwizi arobaini.
(b) Unafikiri kwanini uongozi wa shule aliyokuwa anasoma mwandishi ilipiga vita tabia ya
wanafunzi kusoma wakati wa usiku wa manane.
(c) Una mawazo gani kuhusu kitendo cha Tatu kufuatilia mienendo ya wanafunzi wenzake hasa kwa usiku ule wa manane.
(d) Andika kichwa cha habari kinachofaa kwa habari uliyosoma kisichozidi maneno matano (5).


Ufahamu
2

Soma kwa makini kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali yanayofuata:
Baba alikuwa na wajibu maalum wa kuhakikisha usalama wa familia yake. Ilimbidi awe na nyumba watakamoishi mke na watoto. Nyumba zilijengwa kwa mitindo tofauti katika sehemu mbalimbali hapa nchini. Wanyakyusa walikuwa na ujenzi wao ambao ni tofauti na ule wa Wahaya. Wote wakijenga kwa ufundi wa kuvutia sana. Serikali yetu imehifadhi kwa njia ya makumbusho nyumba zilizojengwa na wakazi wa sehemu mbalimbali hapa nchini wakitumia mitindo yao ya asili. Nyumba hizi zipo katika kijiji cha makumbusho kilichopo nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
Baba akishirikiana na mama walikuwa na wajibu wa kuhakikisha kuwa jamii yao ilipata chakula cha kutosha. Mapema watoto nao walishiriki katika shughuli za kutafuta na kuandaa chakula.
Jamii nyingine hapa nchini zilikuwa zikishughulika na ufugaji tu. Maisha na utajiri wa jamii hizi ulitegemea wanyama. Tangu utoto wao, mafunzo makuu yalihusu ufugaji. Kwa mfano, mtoto wa kimasai alijifunza kuchunga na kulinda wanyama wake tangu utotoni. Ilimbidi awe askari hodari, aweze kupambana na maadui waliotaka kuteka wanyama wao. Alitakiwa aweze kupigana na wanyama wakali porini wenye kuishambulia mifugo. Kumuua simba ilikuwa ni ishara kubwa ya uhodari wa kijana wa kimasai. Mafunzo ya kumwandaa kijana huyo, tangu utoto wake kwa kazi zitakazomkabili katika maisha, yalichukua sehemu kubwa ya malezi.
Kijana wa Kihaya alikabiliwa na mazingira tofauti sana na yale mwenzie wa kimasai. Wahaya ni wakulima, ufugaji ulichukua sehemu ndogo tu katika shughuli zao za kiuchumi. Wahaya hulima mazao ya kudumu kama vile migomba, mashamba yao yalihitaji ulinzi na utunzaji mzuri. Hivyo serikali imara yenye kuhakikisha amani katika nchi ili raia waweze kuendelea na kazi za kilimo kwa amani, ilihitajika. Pia Wahaya walihitaji nyumba za kudumu; maana hali ya maisha yao haikuruhusu uhamaji wa mara kwa mara kama vile Wamasai. Kwa hiyo mafunzo kamili yalihitajika ili kuwaandaa watoto kwa maisha ya namna hiyo.
Maisha katika sehemu mbalimbali katika nchi yalilazimu ziwepo njia maalum za kuwalea,
kuwafundisha na kuwaandaa kwa yale yatakayowakabili katika siku za usoni.

Maswali
(a) Eleza faida mbili zinazoweza kupatikana kwa kuhifadhi mitindo ya nyumba za asili katika kijiji cha makumbusho.
(b) Unafikiri ni sababu gani iliifanya jamii ya Kimasai kuhamahama?
(c) Kwa mujibu wa habari uliyoisoma vijana walikuwa na jukumu gani katika jamii zao?
(d) Andika kichwa cha habari kisichozidi maneno matano kinachofaa kwa habari uliyoisoma.
(e) Andika methali ya Kiswahili inayoendana na aya ya mwisho ya habari uliyoisoma.


Ufahamu
3

Soma kwa makini kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali yanayofuata:
Baba alikuwa na wajibu maalum wa kuhakikisha usalama wa familia yake. Ilimbidi awe na nyumba watakamoishi mke na watoto. Nyumba zilijengwa kwa mitindo tofauti katika sehemu mbalimbali hapa nchini. Wanyakyusa walikuwa na ujenzi wao ambao ni tofauti na ule wa Wahaya. Wote wakijenga kwa ufundi wa kuvutia sana. Serikali yetu imehifadhi kwa njia ya makumbusho nyumba zilizojengwa na wakazi wa sehemu mbalimbali hapa nchini wakitumia mitindo yao ya asili. Nyumba hizi zipo katika kijiji cha makumbusho kilichopo nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam.
Baba akishirikiana na mama walikuwa na wajibu wa kuhakikisha kuwa jamii yao ilipata chakula cha kutosha. Mapema watoto nao walishiriki katika shughuli za kutafuta na kuandaa chakula.
Jamii nyingine hapa nchini zilikuwa zikishughulika na ufugaji tu. Maisha na utajiri wa jamii hizi ulitegemea wanyama. Tangu utoto wao, mafunzo makuu yalihusu ufugaji. Kwa mfano, mtoto wa kimasai alijifunza kuchunga na kulinda wanyama wake tangu utotoni. Ilimbidi awe askari hodari, aweze kupambana na maadui waliotaka kuteka wanyama wao. Alitakiwa aweze kupigana na wanyama wakali porini wenye kuishambulia mifugo. Kumuua simba ilikuwa ni ishara kubwa ya uhodari wa kijana wa kimasai. Mafunzo ya kumwandaa kijana huyo, tangu utoto wake kwa kazi zitakazomkabili katika maisha, yalichukua sehemu kubwa ya malezi.
Kijana wa Kihaya alikabiliwa na mazingira tofauti sana na yale mwenzie wa kimasai. Wahaya ni wakulima, ufugaji ulichukua sehemu ndogo tu katika shughuli zao za kiuchumi. Wahaya hulima mazao ya kudumu kama vile migomba, mashamba yao yalihitaji ulinzi na utunzaji mzuri. Hivyo serikali imara yenye kuhakikisha amani katika nchi ili raia waweze kuendelea na kazi za kilimo kwa amani, ilihitajika. Pia Wahaya walihitaji nyumba za kudumu; maana hali ya maisha yao haikuruhusu uhamaji wa mara kwa mara kama vile Wamasai. Kwa hiyo mafunzo kamili yalihitajika ili kuwaandaa watoto kwa maisha ya namna hiyo.
Maisha katika sehemu mbalimbali katika nchi yalilazimu ziwepo njia maalum za kuwalea,
kuwafundisha na kuwaandaa kwa yale yatakayowakabili katika siku za usoni.

Swali:

Fupisha habari uliyoisoma kwa maneno yasiyozidi mia moja (100).


Ufahamu
4

Soma kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali yanayofuata:
Karibu masikio ya watu wa mahali pengi yalijaa habari za Karama na mashtaka yake. Umaarufu wake wa ghafla ulizungumzwa karibu na mbali. Mtu yeyote wa desturi anapozuka katika umaarufu, huyavuta masikio na macho ya watu wengi kwa sababu jambo kama hili hutokea nadra sana kwa watu ambao bahati mbaya imeshughulika kuwaweka nyuma. Kwa hiyo, siku ya tatu ya baraza ilihudhuriwa na mfalme, watu wenye vyeo mbalimbali, pamoja na nusu moja ya umati mkubwa wa Kusadikika. Fikra zilizochanganyika ziliushika umati huu. Baadhi ya watu walimwajabia Karama
wakamhesabu kama mtu bora wa karne yao. Hawa walitumaini ataokoka lakini wengine waliwaza kuwa Karama alikuwa kama mjinga aliyekuwa akicheza na hatari kubwa iliyofunua taya mbele yake.
Waliokuwa wakimtazamia kuokoka walikuwa na wasiwasi wao; na wale waliokuwa wakimtazamia kuanguka walikuwa na fadhaa yao. Walakini hapana mtu hata mmoja aliyepata kulisema wazo lake.
Bila ya kujua alivyoajabiwa Karama aliendelea kusema mbele ya baraza, “Watu wanaoteswa ndio wanaoyajua mateso yao.” Kusadikika i likuwa c hini ya mateso makubwa sana. Maisha yao yalizungukwa na maradhi na mauti, uadui usiokwisha, nchi iliyokaribia kugeuka jangwa na mwamba na m adhila mengine mazito yaliyowakabili watu. Wanakusadikika walitaka faraja katika mateso haya. Kila jitihada ilijaribiwa ili kuirekebisha saa ya maendeleo ya nchi, lakini mara kwa mara majira yake yalirudishwa nyuma. Kama hili lilifanywa kwa makosa ama kwa makusudi ni siri iliyo ng’ambo ya fahamu zangu hata sasa. Lakini kama siri njema hufichika, ile iliyo mbaya haifichiki hata kidogo. Uchaguzi wa wajumbe ulikuwako lakini hathibitisho ya matokeo ya ujumbe hayakupatikana.
Kusadikika iliishi kuona mjumbe baada ya mjumbe kuadhiriwa n a kuadhibiwa vibaya. Kama washauri hawakudhuriwa na hili lakini watu wengine walidhuriwa sana. Kazi njema za wajumbe wawili zilipotea bure. Manung’uniko ya lawama hii yalikuwa katika hewa yote ya Kusadikika.
Hili lilipotokea serikali iliombwa i ma faima kufanya ujumbe mwingine. Basi mjumbe wa tatu alitakikana ajitolee mwenyewe kwa ujumbe wa Kusini. Wito wa mjumbe wa tatu uliitikiwa na Kabuli; mtu mwenye busara, haya na mcheshi. Yeye alipatikana upesi kabisa kuliko ilivyokuwa kwa mara ya pili na ya kwanza. Misiba ya Buruhani na Fadhili ilikuwa mikubwa ya kutosha kuikongoa mioyo ya bidii katika bawaba zake. Kabuli aliyajua haya yote lakini alikuwa mtu wa moyo wa namna nyingine kabisa. Alikuwa na bidii kubwa kama ile ya siafu athubutiye kukivuka kijito kwa daraja iliyofanywa kwa maiti ya siafu wengine walioelea majini huko na huko. Maji yalijulikana kuwa na asili ya rutuba, mvuke na umeme. Nguvu nyingine za namna mbalimbali zipo pia katika maji. Kama siafu mdudu mdogo na kipofu wakati mwingine haogopi kuzikabili nguvu hizo pamoja na hatari zake kwa sababu njema, basi ni dhahiri kuwa viongozi wa wanadamu wanapoteswa bure bidii za wafuasi wao hutanuka ajabu.
Hapana tishio liwezalo kuukomesha mwendo huu. Kwa hakika utafululiza kuwako duniani mpaka mateso yakome kabisa, na labda wakati huo dunia hii itakuwa njema kama itamaniwavyo kuwa.

Buruhani na Fadhili walitoa sadaka zao bora ili kuyahimiza majilio ya wakati uliotakikana sana. Kabuli aliwaona watu wawili hawa kama wafadhili wakubwa wa ulimwengu. Alitaka kuwa mshirika wao kwa thamani yoyote ya maisha yake.
Kama ilijulikanavyo, Kusini na upande wa dunia yatokako matufani makubwa na baridi kali sana. Kabuli aliyakabili mashaka haya bila ya k igeugeu. Naam, alikuwa kama mtu aliyekuwa akinywa uchungu bila ya kigegezi . Mara mbili alikamatwa akafanywa mahabusu.

Maswali
(a) Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumika katika kifungu cha habari:
(i) Fadhaa
(ii) Madhila
(iii) Kuadhiriwa
(iv) Ima faima
(v) Kigeugeu
(vi) Kigegezi.
(b) Eleza mchanganyiko wa fikira walizonazo wana wa Kusadikika kuhusu Karama.
(c) Kwanini bidii ya mjumbe wa Kusini imelinganishwa na bidii ya siafu? Toa sababu mbili.
(d) Ujumbe wa mwandishi wa kifungu hiki unahusu nini?


Ufahamu
5

Soma kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali yanayofuata:
Karibu masikio ya watu wa mahali pengi yalijaa habari za Karama na mashtaka yake. Umaarufu wake wa ghafla ulizungumzwa karibu na mbali. Mtu yeyote wa desturi anapozuka katika umaarufu, huyavuta masikio na macho ya watu wengi kwa sababu jambo kama hili hutokea nadra sana kwa watu ambao bahati mbaya imeshughulika kuwaweka nyuma. Kwa hiyo, siku ya tatu ya baraza ilihudhuriwa na mfalme, watu wenye vyeo mbalimbali, pamoja na nusu moja ya umati mkubwa wa Kusadikika. Fikra zilizochanganyika ziliushika umati huu. Baadhi ya watu walimwajabia Karama
wakamhesabu kama mtu bora wa karne yao. Hawa walitumaini ataokoka lakini wengine waliwaza kuwa Karama alikuwa kama mjinga aliyekuwa akicheza na hatari kubwa iliyofunua taya mbele yake.
Waliokuwa wakimtazamia kuokoka walikuwa na wasiwasi wao; na wale waliokuwa wakimtazamia kuanguka walikuwa na fadhaa yao. Walakini hapana mtu hata mmoja aliyepata kulisema wazo lake.
Bila ya kujua alivyoajabiwa Karama aliendelea kusema mbele ya baraza, “Watu wanaoteswa ndio wanaoyajua mateso yao.” Kusadikika i likuwa c hini ya mateso makubwa sana. Maisha yao yalizungukwa na maradhi na mauti, uadui usiokwisha, nchi iliyokaribia kugeuka jangwa na mwamba na m adhila mengine mazito yaliyowakabili watu. Wanakusadikika walitaka faraja katika mateso haya. Kila jitihada ilijaribiwa ili kuirekebisha saa ya maendeleo ya nchi, lakini mara kwa mara majira yake yalirudishwa nyuma. Kama hili lilifanywa kwa makosa ama kwa makusudi ni siri iliyo ng’ambo ya fahamu zangu hata sasa. Lakini kama siri njema hufichika, ile iliyo mbaya haifichiki hata kidogo. Uchaguzi wa wajumbe ulikuwako lakini hathibitisho ya matokeo ya ujumbe hayakupatikana.
Kusadikika iliishi kuona mjumbe baada ya mjumbe kuadhiriwa n a kuadhibiwa vibaya. Kama washauri hawakudhuriwa na hili lakini watu wengine walidhuriwa sana. Kazi njema za wajumbe wawili zilipotea bure. Manung’uniko ya lawama hii yalikuwa katika hewa yote ya Kusadikika.
Hili lilipotokea serikali iliombwa i ma faima kufanya ujumbe mwingine. Basi mjumbe wa tatu alitakikana ajitolee mwenyewe kwa ujumbe wa Kusini. Wito wa mjumbe wa tatu uliitikiwa na Kabuli; mtu mwenye busara, haya na mcheshi. Yeye alipatikana upesi kabisa kuliko ilivyokuwa kwa mara ya pili na ya kwanza. Misiba ya Buruhani na Fadhili ilikuwa mikubwa ya kutosha kuikongoa mioyo ya bidii katika bawaba zake. Kabuli aliyajua haya yote lakini alikuwa mtu wa moyo wa namna nyingine kabisa. Alikuwa na bidii kubwa kama ile ya siafu athubutiye kukivuka kijito kwa daraja iliyofanywa kwa maiti ya siafu wengine walioelea majini huko na huko. Maji yalijulikana kuwa na asili ya rutuba, mvuke na umeme. Nguvu nyingine za namna mbalimbali zipo pia katika maji. Kama siafu mdudu mdogo na kipofu wakati mwingine haogopi kuzikabili nguvu hizo pamoja na hatari zake kwa sababu njema, basi ni dhahiri kuwa viongozi wa wanadamu wanapoteswa bure bidii za wafuasi wao hutanuka ajabu.
Hapana tishio liwezalo kuukomesha mwendo huu. Kwa hakika utafululiza kuwako duniani mpaka mateso yakome kabisa, na labda wakati huo dunia hii itakuwa njema kama itamaniwavyo kuwa.

Buruhani na Fadhili walitoa sadaka zao bora ili kuyahimiza majilio ya wakati uliotakikana sana. Kabuli aliwaona watu wawili hawa kama wafadhili wakubwa wa ulimwengu. Alitaka kuwa mshirika wao kwa thamani yoyote ya maisha yake.
Kama ilijulikanavyo, Kusini na upande wa dunia yatokako matufani makubwa na baridi kali sana. Kabuli aliyakabili mashaka haya bila ya k igeugeu. Naam, alikuwa kama mtu aliyekuwa akinywa uchungu bila ya kigegezi . Mara mbili alikamatwa akafanywa mahabusu.

Swali:

Fupisha habari uliyosoma hapo juu kwa maneno yasiyopungua mia moja na hamsini
(150) na yasiozidi mia mbili (200).


Ufahamu
6

Soma kwa makini kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali yanayofuata.
Ustaarabu ni jambo jema ambalo hupendwa na kila jamii yenye utashi hapa duniani. Kila jamii yenye ustaarabu mambo yake huendeshwa kwa kuzingatia kanuni na taratibu zinazoeleweka.
Maamuzi na mafanikio mbalimbali miongoni mwa wanajamii hutolewa bila hamaki wala
kukurupuka. Kanuni na taratibu hizo huiongoza jamii kufikia upeo wake kimaendeleo kuanzia ngazi za chini kabisa ambayo ni familia mpaka ngazi ya juu kabisa ambayo ni taifa. Taratibu na kanuni hizo huwekwa katika chombo kimoja maalumu kinachoitwa katiba.
Katiba ni jumla ya sheria, kanuni na taratibu fulani zilizokubaliwa kuwekwa na jamii au taifa fulani kama dira ya maisha ya kila siku ya jamii au taifa hilo. Taifa bila katiba ni sawa na behewa la garimoshi bila injini. Hivyo katiba ina umuhimu wa kipekee katika taifa lolote lile.
Katika nchi zenye utamaduni wa kidemokrasia, katiba huundwa kutokana na maoni ya wananchi wake kwa utaratibu maalumu uliowekwa na serikali. Aghalbu, maoni na mawazo yaliyotolewa na wananchi huwa ni chimbuko la katiba hiyo. Wananchi hujiona ni sehemu ya utawala. Kwa upande wa pili wa sarafu, nchi zenye utaratibu wa kiimla , katiba hutayarishwa na watawala kwa maslahi yao binafsi. Katiba hutumiwa kama sera kwa maslahi ya watawala. Maoni na mawazo ya wananchi hayazingatiwi katika kuunda katiba.
Umuhimu wa katiba huonekana na kujidhihirisha waziwazi katika maisha ya kila siku ya nchi yoyote ile. Kwanza, katiba huelekeza wajibu wa ila mwanajamii kwa taifa lake na wajibu wa viongozi walio madarakani kwa wananchi au raia. Pili, katiba huonesha na kuainisha haki ambazo kila raia anastahili kupata na pia taratibu za kufuata katia kudai au dupewa haki hizo.

Mbali na hayo, katiba hutoa utaratibu wa jinsi ya kuwapata viongozi wetu katika ngazi mabalimbali za kisiasa na kijamii. Pia uhuru wa mtu binafsi hulindwa na katiba. Hivyo, katika nchi ambayo ina katiba inayokidhi matarajio ya wananchi wote mambo huwa mazuri na kamwe chombo hakiwezi kwenda mrama .
Aidha, wananchi hawana budi kuelewa maana ya katiba ili waweze kutoa maoni na mapendekezo ya kuunda katiba mpya au kuimarisha iliyopo. Ni muhali kwa mtu asiyejua maana ya katiba kutoa maoni kuhusu katiba. Wananchi hupaswa kuelimishwa kupita semina, warsha na makongamano mbalimbali ili kujua katiba zao na kutoa maoni kuhusu uundaji wa katibu mpya.
Hata hivyo, wananchi wengi hasa vijana hawajitumi katika kuzijua katiba za nchi zao au kutoa maoni ya uundaji wa katiba mpya. Athari zake ni kutojua haki zao za msingi na kuburutwa kama mkokoteni na watawala katika mambo mbalimbali. Vilevile hulalamikia mambo ambayo hawakuchangia mawazo.
Hivyo basi, ni vizuri kwa wananchi kutambua, kuthamini na kuheshimu uwepo wa katiba kama kiongozi kizuri katika kuonesha njia muafaka ya kujiletea maendeleo kisiasa, kijamii, kiuchumi na kiutamaduni kwa nchi husika.

Maswali
(a) Toa maana ya maneno yote yaliyokolezwa wino kama yalivyotumika katika habari uliyosoma.
(b) Kwa mujibu wa habari uliyosoma, taja mambo mazuri mawili yatokanayo na uwepo wa katiba katika nchi.
(c) Kwanini mwandishi anasema katiba hutumiwa kama sera kwa maslahi ya watawala?
(d) Je, ni hofu gani aliyonayo mwandishi dhidi ya vijana kuhusu katiba?
(e) Andika kichwa cha habari uliyosoma kisichozidi maneno matano (5).


Ufahamu
7

Soma kwa makini kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali yanayofuata.
Ustaarabu ni jambo jema ambalo hupendwa na kila jamii yenye utashi hapa duniani. Kila jamii yenye ustaarabu mambo yake huendeshwa kwa kuzingatia kanuni na taratibu zinazoeleweka.
Maamuzi na mafanikio mbalimbali miongoni mwa wanajamii hutolewa bila hamaki wala
kukurupuka. Kanuni na taratibu hizo huiongoza jamii kufikia upeo wake kimaendeleo kuanzia ngazi za chini kabisa ambayo ni familia mpaka ngazi ya juu kabisa ambayo ni taifa. Taratibu na kanuni hizo huwekwa katika chombo kimoja maalumu kinachoitwa katiba.
Katiba ni jumla ya sheria, kanuni na taratibu fulani zilizokubaliwa kuwekwa na jamii au taifa fulani kama dira ya maisha ya kila siku ya jamii au taifa hilo. Taifa bila katiba ni sawa na behewa la garimoshi bila injini. Hivyo katiba ina umuhimu wa kipekee katika taifa lolote lile.
Katika nchi zenye utamaduni wa kidemokrasia, katiba huundwa kutokana na maoni ya wananchi wake kwa utaratibu maalumu uliowekwa na serikali. Aghalbu, maoni na mawazo yaliyotolewa na wananchi huwa ni chimbuko la katiba hiyo. Wananchi hujiona ni sehemu ya utawala. Kwa upande wa pili wa sarafu, nchi zenye utaratibu wa kiimla , katiba hutayarishwa na watawala kwa maslahi yao binafsi. Katiba hutumiwa kama sera kwa maslahi ya watawala. Maoni na mawazo ya wananchi hayazingatiwi katika kuunda katiba.
Umuhimu wa katiba huonekana na kujidhihirisha waziwazi katika maisha ya kila siku ya nchi yoyote ile. Kwanza, katiba huelekeza wajibu wa ila mwanajamii kwa taifa lake na wajibu wa viongozi walio madarakani kwa wananchi au raia. Pili, katiba huonesha na kuainisha haki ambazo kila raia anastahili kupata na pia taratibu za kufuata katia kudai au dupewa haki hizo.

Mbali na hayo, katiba hutoa utaratibu wa jinsi ya kuwapata viongozi wetu katika ngazi mabalimbali za kisiasa na kijamii. Pia uhuru wa mtu binafsi hulindwa na katiba. Hivyo, katika nchi ambayo ina katiba inayokidhi matarajio ya wananchi wote mambo huwa mazuri na kamwe chombo hakiwezi kwenda mrama .
Aidha, wananchi hawana budi kuelewa maana ya katiba ili waweze kutoa maoni na mapendekezo ya kuunda katiba mpya au kuimarisha iliyopo. Ni muhali kwa mtu asiyejua maana ya katiba kutoa maoni kuhusu katiba. Wananchi hupaswa kuelimishwa kupita semina, warsha na makongamano mbalimbali ili kujua katiba zao na kutoa maoni kuhusu uundaji wa katibu mpya.
Hata hivyo, wananchi wengi hasa vijana hawajitumi katika kuzijua katiba za nchi zao au kutoa maoni ya uundaji wa katiba mpya. Athari zake ni kutojua haki zao za msingi na kuburutwa kama mkokoteni na watawala katika mambo mbalimbali. Vilevile hulalamikia mambo ambayo hawakuchangia mawazo.
Hivyo basi, ni vizuri kwa wananchi kutambua, kuthamini na kuheshimu uwepo wa katiba kama kiongozi kizuri katika kuonesha njia muafaka ya kujiletea maendeleo kisiasa, kijamii, kiuchumi na kiutamaduni kwa nchi husika.

 

Swali:

Fupisha habari uliyosoma kwa maneno yasiyopungua mia moja (100).


Ufahamu
8

Soma shairi lifuatalo kisha jibu maswali yanayofuata:
Ima mwana wende kasi, ima usirudi nyuma
Ima ukwepe sabasi, ima ukipite kima
Ima ujivike lasi, ima ndiyo taadhima
Ima mwanakwetu ima, dunia ni sarakasi.


Ima kasema mkwasi , ima uende kulima
Ima njaa sikughasi, ima mgongo inama
Ima wepuke uasi, ima upate usalama
Ima mwanakwetu ima, ima ndipo utapasi.


Ima ndipo utapasi , ima mwanakwetu ima
Ima ujiunge nasi, ima tuujenge umma
Ima usile najisi, ima ule cha kuchuma
Ima mwanakwetu ima, ima emaye hakosi.


Ima emaya hakosi, ima jikalifu ima
Ima upweke tatasi, ima wewe na Mwajuma
Ima yoyomea kusi, ima usiuye nyuma
Ima wa ima faima, ima upate fulusi.


Ima wmanakwetu basi, ima usende kinyuma
Ima kazi ni libasi , ima inama kulima
Ima wacha udadisi, ima nakwambia ima
Ima usikae ima, kama kuishi wahisi.

Maswali
(a) Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumika katika shairi ulilolisoma:
(i) Mkwasi
(ii) Utapasi
(iii) Jikalifu
(iv) Libasi
(b) Kwa kutumia sentensi tatu (3), fafanua ujumbe wa mwandishi katika shairi hili.
(c) Msanii ana maana gani anaposema “Ima mwanakwetu ima, dunia ni sarakasi.”


Ufahamu
9

Soma kifungu cha habari kifuatacho kisha fupisha habari hii kwa maneno hamsini (50).
Kijana anahitaji kuwa na rafiki ili aweze kuondokana na ukiwa pia ili aweze kupata faraja. Aidha hayo yatajitokeza kwa sababu atafahamiana na marafiki hao, vilevile atazoeana nao hasa kwa kupitia maongezi. Kijana huweza kupata marafiki popote, kwa mfano miongoni mwa majirani zake, shuleni, kazini, sehemu za ibada na hata awapo safarini. Lakini kijana anapaswa kuwa mwangalifu katika kuchagua marafiki.
Katika makuzi yake kijana huwa karibu sana na rafiki zake ambao kwa kiasi kikubwa huwa na nguvu na ni rahisi kwa rafiki kuambukizana tabia ambazo zaweza kuwa nzuri au mbaya. Kwa hiyo ni jukumu la wazazi kumwelekeza kijana na kumshauri kuhusu ni yupi hasa rafiki mwema. Ni heri kukosa rafiki kuliko kuwa na rafiki mlevi, mwongo, mwizi, mvivu, mvuta bangi au mtumiaji wa dawa za kulevya. Rafiki mzuri ni yule mwenye tabia njema na busara ambaye hutoa ushauri mzuri unaoweza kumsaidia mtu kupata mafanikio katika maisha.


Ufahamu
10

Soma​ ​ kifungu​ ​ cha​ ​ habari​ ​ kifuatacho​ ​ kisha​ ​ jibu​ ​ maswali​ ​ yanayofuata.

Suala la kuwapenda na kuwajali watoto ni muhimu sana kaitka jamii. Leo hii suala la kuwaonesha watoto mapenzi limekuwa na jambo la ziada kwa watu na familia nyingi. Kuna mambo mengine mengi​ ​ maishani​ ​ mwetu​ ​ ambayo​ ​ watu​ ​ wengi​ ​ huyaona​ ​ kuwa​ ​ muhimu​ ​ zaidi​ ​ badala​ ​ ya​ ​ watoto.

Kuna vitendo vingi vya ukatili ambavyo watoto hutendewa. Hivi majuzi kumekuwa na visa vya watoto wengi wachanga kutupwa majalalani. Viumbe hawa walipokatiziwa uhai, maiti zao zilitupwa kama takataka na hiyo ni miili ambayo ilipatikana jalalani. Lakini wengi wanajiuliza kuna maelfu mangapi ya miili mingine kama hiyo inayotupwa? Hili lilikuwa tone dogo la bahari ya dhambi ambazo sote tunaogelea ndani. Ni vema kila mtu kwa nafasi yake katika jamii, kuwaokoa watoto
wetu,​ ​ ili​ ​ tusije​ ​ tukawalilia​ ​ baadaye.


Mambo kama haya ni mazao ya mimiea yetu ambayo tuliipanda sisi ambao hutachelewi kujiita watu walio huru, walio na maendeleo na wa kisasa. Tumekuwa watu wa kupuuza mambo ya kimapokeo ya kuzingatia utu na kuficha aibu. Aghalabu tumejitia usasa kwa kutazama filamu na video zisizokuwa na maadili, kusikiliza muziki wenye maneno yasiyokuwa na maadili. Tunapoona watoto wetu wakitembea nusu uchi, hatushughuliki hata kidogo kuwakanya na matokeo yake ni hapo
tulipofikia sasa. Kama ni kosa, sisi sote tumehusika kwa njia moja au nyingine. Ni vizuri tuelewe kuwa​ ​ sisi​ ​ ni​ ​ watunzaji​ ​ na​ ​ walezi​ ​ wa​ ​ ndugu​ ​ zetu​ ​ kwa​ ​ kila​ ​ njia.


Tutawaokoa watoto kwa kukataa mambo yote yanayowanyanyasa. Lazima tuwaoneshe watoto mapenzi. Mapenzi si chakula, mavazi na makazi tu. Mapenzi si kuwaachia vijana uhuru watende wapendavyo. Mapenzi sio kuwanunulia vitu vya bei ghali au kuacha kuwakemea wanapokosa mwelekeo. Mapenzi kwa watoto ni kuwaheshimu na kuwatendea kama binadamu yeyote. Lazima mzazi akumbuke kwamba mtoto hujifunza kutoka kwake. Mtoto atamtendea mzazi jinsi alivyotendwa. Aidha, jinsi mzazi anavyomtendea mtoto wake ndivyo atakavyowatendea watoto
wake​ ​ na​ ​ wale​ ​ wote​ ​ ambao​ ​ atapata​ ​ kuhusiana​ ​ nao​ ​ kwa​ ​ njia​ ​ moja​ ​ au​ ​ nyingine.


Wazazi ni lazima wawaokoe watoto wao katika viwango vyote vya ukuaji, kusiwe na mwanya baina ya mzazi na mtoto. Watoto waweze kuwaambia wazazi yote yanayowahangaisha mioyoni mwao, na hali hii itawapa wazazi fursa ya kuwasaidia. Mtoto anapokosa wazazi wawe tayari kumwonesha kosa​ ​ lake​ ​ na​ ​ kumwadhibu​ ​ kwa​ ​ mapenzi.


Mtoto mwingine yeyote akipotoka wazazi wawe tayari kumkosoa na kuwaarifu wazazi wake.Tuache ubinafsi wetu, tukumbuke kuwa mwana wa mwenzio ni wako pia. Ni jambo la busara kuhaikikisha​ ​ kwamba​ ​ kama​ ​ wazazi,​ ​ tuzingatie​ ​ haki​ ​ zote​ ​ za​ ​ watoto.

Maswali
1. (a) Pendekeza​ ​ kichwa​ ​ kinachofaa​ ​ kwa​ ​ habari​ ​ hii​ ​ kisichozidi​ ​ maneno​ ​ manne.
(b) Fafanua​ ​ chanzo​ ​ cha​ ​ mienendo​ ​ isiyofaa​ ​ kwa​ ​ vijana​ ​ kama​ ​ kilivyoelezwa​ ​ na​ ​ mwandishi.
(c) Kwa​ ​ nini​ ​ mwandishi​ ​ anasema​ ​ sisi​ ​ sote​ ​ tumehusika​ ​ na​ ​ mienendo​ ​ mibaya​ ​ ya​ ​ watoto​ ​ wetu?
(d) Mwandishi​ ​ anatoa​ ​ msimamo​ ​ gani​ ​ kwa​ ​ wazazi​ ​ kuhusu​ ​ suala​ ​ la​ ​ mapenzi​ ​ katika​ ​ malezi​ ​ ya​ ​ watoto wetu.
(e) “Mtoto​ ​ wa​ ​ mwenzetu​ ​ akipotoka,​ ​ pia​ ​ tuwe​ ​ tayari​ ​ kumkosoa.”​ ​ Unafikiri​ ​ kwa​ ​ mazingira​ ​ ya​ ​ sasa inawezekana?​ ​ Toa​ ​ maoni​ ​ yako.

2. Fupisha​ ​ habari​ ​ uliyosoma​ ​ kwa​ ​ maneno​ ​ mia​ ​ moja​ ​ (100).


Ufahamu