Warning: Undefined array key 1 in /home/acaproso/public_html/._System/._Template/.Main.php on line 116
Ufahamu questions

Ufahamu questions | form four Kiswahili

Find Ufahamu examination questions, form four Kiswahili in acaproso.com

# Question
1

Soma kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali kwa kuandika herufi ya jibu sahihi kando ya namba ya swali.
Nisubiri! Nisubiri nini? Sikupewa talaka. Nilitelekezwa. Jani linapeperushwa lakini hakuna mkono wowote unaothubutu kuliokota, kama vile ambavyo angesema nyanya yangu.
Hata hivyo niliishi. Niliyajua matatizo ya usafiri yaliyokuwepo. Wanangu walikwenda shuleni kwa taabu lakini walivumilia na kuchekelea. Siku moja nikamsikia dada akiwashauri. "Hasa! Msimwambie mama jinsi watu wanavyobanana mwenye magari wakati wa kwenda na kurudi kazini".
Nililia kwa furaha iliyochanganyika na huzuni. Nilifurahi kwa vile nilipendwa na wanangu na
nilihuzunika kwa vile sikuwa na uwezo wa kuikabili hali halisi iliyokuwepo. Kwa hiyo nilikueleza bila kukuficha hali hiyo ya kuhuzunisha ya maisha yetu. Wakati ambapo bibi mamamkwe alikuwa akizitembelea pembe zote za mji akitumia gari la Modu, na Binetuu alikuwa akitamba katika barabara zote akiendesha gari la aina ya Alfa Romeo, mara jekundu mara jeupe.
Sitasahau kamwe jamala uliyonifanyia wewe, dada yangu. Wala sitasahau kamwe furaha na mshangao nilioupata wakati ambapo muuzaji wa magari ya aina ya Fiat aliponiita na kuniambia nichague gari nililotaka, na kwamba wewe ungegharimia kila kitu. Wanangu walishangilia kwa furaha walipotambua kwamba mahangaiko yao yalikuwa karibu kumalizika, mahangaiko wayapatayo wanafunzi wengi sana kila siku.
Katika urafiki, mna upendo mkuu usiojulikana. Huwa unakomaa wakati wa matatizo. Lakini ukali uliozidi mno huua upendo. Urafiki hukaa imara katika nyakati zinazochosha na kuudhi na kuwatenganisha waliooana. Ama kwa hakika katika urafiki mna upendo uliolenga juu kabisa kusikojulikana. Wewe sonara ulijinyima na ukaweza kunisaidia wakati wa dhiki.
Nikajifunza kuendesha na nikautawala woga wangu. Hii nafasi ndogo iliyoko kati ya usukani na kiti cha mbele ikawa yangu. Ninapokanyaga klachi mwendo unaongezeka. Nikikanyaga breki mwendo unapungua, na ninapotaka kwenda kasi nakanyaga akselereta. Nilijivunia akselereta. Nilipoikanyaga kidogo tu gari ilichanganya mwendo mkali. Miguu yangu ikajifunza kuchezecheza juu ya hizo pedali. Wakati nilipokuwa nimekata tamaa kabisa nilikuwa najisemea mwenyewe: "Kwa nini Binetuu aendeshe gari na siyo mimi? Tena niliwaza." Nisimdanganye Aisatu! Niliishinda hiyo vita ya mishipa ya fahamu na ya kujishinda binafsi. Niliipata leseni ya kuendesha na nilikufahamisha.
Nilikueleza, na sasa je? Wanangu wakiwa wamestarehe kwenye kiti cha nyuma ya gari yangu aina ya Fiat 125, rangi ya maziwa, ambayo uliniletea wanaweza kumwangalia kwa dharau yule mke mwenzangu.

Maswali
(i) Mwandishi wa habari hii ana matatizo ya
A kupewa talaka na mumewe
B umaskini uliokithiri
C kutelekezwa na mumewe
D kutokuwa na usafiri
E kuwa na watoto wengi.
(ii) Binetuu ni
A rafiki yake mwandishi
B bibi mkwe wake mwandishi
C mke mwenzie mwandishi
D hawana uhusiano wowote
E jirani wa mwandishi.
(iii) Mwandishi anaposema “katika urafiki mna upendo mkuu … unakomaa wakati wa matatizo”,
anamaanisha kuwa
A akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli
B rafiki wa kweli ni yule anayekupenda wakati wa dhiki tu
C kila shetani na mbuyu wake
D huruma ya kweli inapatikana wakati wa dhiki
E rafiki ni yule mwenye upendo wa chati.
(iv) Nyanya kama lilivyotumiwa na mwandishi maana yake ni
A tunda linaloungwa kwenye mboga B rafiki mzee
C mama wa mzazi wako D ajuza
E yote si kweli.
(v) Kulingana na habari hii kuna vitu vitatu muhimu vinavyotumika wakati wa kuendesha gari.
Navyo ni:
A Usukani, breki na klachi
B Kiti cha dereva, klachi na akselereta
C Pedali, klachi na breki
D Klachi, akselereta na breki
E Akselereta na breki.
(vi) Neno “jamala” kama ilivyotumiwa na mwandishi linamaanisha
A wema wako B juhudi zako
C rehema zako D upendo wako
E upole wako.
(vii) Kulingana na habari hii Modu ni
A jina la mume wa mwandishi
B aina ya gari
C halijulikani maana yake
D majibu yote si kweli
E ni rafiki wa sonara.

(viii) Rafiki yake mwandishi kazi yake ni
A sonara
B mfanyabiashara
C muuza magari
D afisa
E dereva.
(ix) Sifa za watoto wa mwandishi kulingana na habari hii ni
A wenye upendo, huruma, wavumilivu na wapole
B wavumilivu na wenye furaha wakati wote
C wakaidi na wanaocheka ovyo
D wakaidi kwa majirani na marafiki
E sifa zote hizo wanazo.
(x) Mwandishi anazungumzia matatizo yanayowakumba wanawake
A katika jamii
B wasio na upendo
C waliotelekezwa na waume zao
D walioachiwa watoto kuwalea peke yao
E wote wenye ndoa.


Ufahamu
2

Soma kifungu cha habari kifuatacho kisha andika ufupisho wa maneno 60 kuhusu habari hiyo.
Vijana popote duniani ni tegemeo la taifa. Kupuuza malezi ya vijana ni sawa na kupuuza uhai wa taifa. Leo hii tukitazama mwelekeo wa malezi ya watoto wetu, ipo hali ya kutatanisha sana. Sasa hivi malezi ya watoto hasa katika jumuiya yetu hapa Tanzania, yamekuwa na ugumu wa pekee. Baadhi ya vijana wetu wamejiingiza katika mambo ya aibu, mfano ulevi, uvutaji bangi, mambo ya ngono na vitendo vingine viovu. Sasa hivi baadhi yao hawana aibu tena na wanayumba maishani. Wengine wanapenda maisha ya starehe, njia za kujipatia mali haraka haraka na mengine mengi ya kusikitisha.
Tukumbuke kwamba hawa ndio wataiongoza nchi wakati wazee wao watakapomaliza muda wao wa kuishi hapa duniani. Lakini hebu tujiulize swali moja. Ni nani alaumiwe? Je tuwalaumu watoto? Tuwalaumu wazazi au nani?
Mambo ya burudani yalikuwepo tangu zamani lakini yalikuwa na mipaka yake. Mathalani ilikuwa ni mwiko kwa vijana wa kike kutembea peke yao, walitembea katika vikundi.
Tendo la kuzaa nje ya ndoa lilikuwa likilaumiwa vikali na ilikuwa ni aibu kwa binti yeyote
kukumbwa na balaa kama hilo.


Ufahamu
3

Soma habari ifuatayo kwa makini na kisha jibu maswali yanayofuata:
Wimbi la kusakama wahamiaji kutoka nchi jirani, hasa vijana wenye kazi, limeshika kasi katika miji mbalimbali nchini Afrika Kusini. Watu arobaini wameripotiwa kuuawa hadi sasa, mamia wamejeruhiwa, baadhi wakiwa wamechomwa moto. Vijana wenye mapanga, visu, nondo, nyundo na mishale wanawasaka mahamiaji majumbani, ofisini na mitaani.
Ghasia hizo zinatokana na vijana wa Afrika kusini kudai kwamba wanakosa ajira kwa sababu nafasi zao zinachukuliwa na wageni na wao kubaki wanazurura mitaani bila ya kazi. Wimbi hilo la vurugu na mauaji limeiharibia sifa Afrika Kusini nchi ambayo ilifikia hapo ilipo kwa msaada mkubwa wa hali na mali wa nchi za kusini mwa Afrika. Watu wa Afrika Kusini wamesahau kwamba wakati wa utawala wa makaburu, nchi jirani ziliwapokea maelfu kwa maelfu ya vijana na wazee wa Afrika Kusini kuwapa hifadhi pamoja na kusaidia mikakati ya mapambano dhidi ya makaburu. Pia vijana wa nchi hizo walikosa nafasi za masomo ya juu kutokana na wakimbizi wa Afrika Kusini kupewa upendeleo katika shule za sekondari na vyuo vikuu vya nchi hizo. Lakini leo hii watu wa nchi hizi wanaonekana si lolote si chochote nchini Afrika ya Kusini.
Hivi sasa vijana wengi wamekosa ajira katika nchi za Zimbabwe, Msumbiji, Malawi na hata
Tanzania kwa vile makampuni ya Afrika ya Kusini yamechukua makampuni makubwa ya nchi hizo kama vile viwanda vya bia, mabenki na huajiri watu kutoka Afrika Kusini kufanya kazi huko. Suala hilo limehamasisha kukimbilia Afrika Kusini kwa vijana wengi ili kupata ajira.
Sasa njia pekee iliyobaki kwa vijana wa nchi jirani wasiokuwa na kazi ni kuzifuata ajira hizo Afrika Kusini. Wageni, hasa kutoka nchi za Afrika, wamekuwa wakikutana na vikwazo vya kupata vibali vya kufanya kazi, lakini wamekuwa wakitumia njia za panya kupata ajira. Vijana wengi wa Afrika Kusini wamekuwa wakikosa ajira kutokana na elimu ndogo au maambukizi ya virusi vya UKIMWI yaliyozagaa nchini humu ukilinganisha na nchi jirani.
Takwimu za serikali, kwa mfano, zinaonesha zaidi ya asilimia thelathini (30%) ya wafanyakazi wa kwenye bandari ya mji wa Durban na maeneo ya ukanda wa Pwani, wanaishi na virusi vya UKIMWI na makampuni ya maeneo hayo yamekuwa yakibagua katika ajira maana uwezo wa watu hao kufanya kazi za sulubu ni mdogo kwa sababu ya UKIMWI.
Kwa ujumla ghasia zimezusha wasiwasi mkubwa kwa Afrika Kusini, nchi ambayo inakabiliwa na maandalizi ya kuwa mwenyeji wa michuano ya fainali za Kombe la Dunia kwa mchezo wa soka mwaka 2010. Inatarajiwa kuvutia wageni wapatao nusu milioni. Wasiwasi unakuja kwa vile kiasi kikubwa cha fedha kimetumika katika maandalizi na faida yake inatarajiwa kupatikana wakati wa mashindano hayo. Hivyo vitendo vya mauaji vinatia doa. Upo uwezekano wa kukosa nafasi hiyo kutokana na kuhofia usalama na amani kwa wanamichezo.

Maswali
(a) Kichwa cha habari hii kinachofaa ni kipi?
(b) Vijana wengi kusini mwa Afrika wamemiminika Afrika Kusini ili wapate ajira. Eleza mambo
mawili (2) yaliyosababisha vijana hao wapate ajira Afrika ya Kusini.
(c) Ungeishauri nini serikali ya Afrika ya Kusini?
(d) Makampuni yanahofia kuwaajiri vijana wa Afrika Kusini. Ipi sababu kubwa ya hofu hiyo?


Ufahamu
4

Soma habari ifuatayo kwa makini na kisha jibu maswali yanayofuata:
Wimbi la kusakama wahamiaji kutoka nchi jirani, hasa vijana wenye kazi, limeshika kasi katika miji mbalimbali nchini Afrika Kusini. Watu arobaini wameripotiwa kuuawa hadi sasa, mamia wamejeruhiwa, baadhi wakiwa wamechomwa moto. Vijana wenye mapanga, visu, nondo, nyundo na mishale wanawasaka mahamiaji majumbani, ofisini na mitaani.
Ghasia hizo zinatokana na vijana wa Afrika kusini kudai kwamba wanakosa ajira kwa sababu nafasi zao zinachukuliwa na wageni na wao kubaki wanazurura mitaani bila ya kazi. Wimbi hilo la vurugu na mauaji limeiharibia sifa Afrika Kusini nchi ambayo ilifikia hapo ilipo kwa msaada mkubwa wa hali na mali wa nchi za kusini mwa Afrika. Watu wa Afrika Kusini wamesahau kwamba wakati wa utawala wa makaburu, nchi jirani ziliwapokea maelfu kwa maelfu ya vijana na wazee wa Afrika Kusini kuwapa hifadhi pamoja na kusaidia mikakati ya mapambano dhidi ya makaburu. Pia vijana wa nchi hizo walikosa nafasi za masomo ya juu kutokana na wakimbizi wa Afrika Kusini kupewa upendeleo katika shule za sekondari na vyuo vikuu vya nchi hizo. Lakini leo hii watu wa nchi hizi wanaonekana si lolote si chochote nchini Afrika ya Kusini.
Hivi sasa vijana wengi wamekosa ajira katika nchi za Zimbabwe, Msumbiji, Malawi na hata
Tanzania kwa vile makampuni ya Afrika ya Kusini yamechukua makampuni makubwa ya nchi hizo kama vile viwanda vya bia, mabenki na huajiri watu kutoka Afrika Kusini kufanya kazi huko. Suala hilo limehamasisha kukimbilia Afrika Kusini kwa vijana wengi ili kupata ajira.
Sasa njia pekee iliyobaki kwa vijana wa nchi jirani wasiokuwa na kazi ni kuzifuata ajira hizo Afrika Kusini. Wageni, hasa kutoka nchi za Afrika, wamekuwa wakikutana na vikwazo vya kupata vibali vya kufanya kazi, lakini wamekuwa wakitumia njia za panya kupata ajira. Vijana wengi wa Afrika Kusini wamekuwa wakikosa ajira kutokana na elimu ndogo au maambukizi ya virusi vya UKIMWI yaliyozagaa nchini humu ukilinganisha na nchi jirani.
Takwimu za serikali, kwa mfano, zinaonesha zaidi ya asilimia thelathini (30%) ya wafanyakazi wa kwenye bandari ya mji wa Durban na maeneo ya ukanda wa Pwani, wanaishi na virusi vya UKIMWI na makampuni ya maeneo hayo yamekuwa yakibagua katika ajira maana uwezo wa watu hao kufanya kazi za sulubu ni mdogo kwa sababu ya UKIMWI.
Kwa ujumla ghasia zimezusha wasiwasi mkubwa kwa Afrika Kusini, nchi ambayo inakabiliwa na maandalizi ya kuwa mwenyeji wa michuano ya fainali za Kombe la Dunia kwa mchezo wa soka mwaka 2010. Inatarajiwa kuvutia wageni wapatao nusu milioni. Wasiwasi unakuja kwa vile kiasi kikubwa cha fedha kimetumika katika maandalizi na faida yake inatarajiwa kupatikana wakati wa mashindano hayo. Hivyo vitendo vya mauaji vinatia doa. Upo uwezekano wa kukosa nafasi hiyo kutokana na kuhofia usalama na amani kwa wanamichezo.

Swali:

Andika ufupisho wa aya mbili za mwisho za habari uliyoisoma kwa maneno hamsini (50) .


Ufahamu
5

Soma kwa makini kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali yatakayofuata:
Kwa neno zima uzalendo ni mapenzi ya nchi. Mapenzi haya hayafanyiki kwa njia za kubuniwa na watu lakini yamekwishatangulia kuwa katika mioyo yetu. Uzalendo ni tabia ya maumbile, nasi tunayo toka wakati wa kuzaliwa. Tunafikiri habari za nchi yetu kama tufikiriavyo habari za baba na mama zetu; kwa hivi kila mtu anajali sana mahali alipozaliwa.
Baadhi ya watu hawakubali nao wako tayari siku zote kupinga pishi ya hoja zako kwa ukufi wa hoja zao. Wao hufikiri kwamba uzalendo ni maono ya ushupavu na dalili ya uchache wa ustaarabu wa moyo. Kwao uzalendo ni imani ya kishenzi, kwa sababu hutenga kando nchi nyingine.
Wanadai kwamba mtu ni lazima apende ulimwengu mzima na watu wa ulimwengu hufanya kila mtu kuwa raia wa dunia si wa mahali pake padogo pajulikanapo kama nchi yake. Lazima niseme kweli kwamba wazo la udugu wa ulimwengu ni bora kwa makisio lakini kwa matumizi haliwezekani. Bora katika watu ni yule apendaye nchi yake kwanza. Kuna mashaka makubwa kama mtu anaweza kuamini katika mapenzi ya udugu wa ulimwengu bila kupenda nchi yake ikiwa hivyo, uzalendo huthibitisha ubora wa kupenda sehemu ya ulimwengu ambayo ndani yake tumezaliwa.
Mapenzi ya mtu kwa nchi yake hayaoneshi chuki ya nchi nyingine za ulimwengu. Uzalendo wa uwongo ndiyo utufanyao kuchukia nchi nyingine. Aidha, lazima tupende nchi zetu kwa sababu ya nchi zenyewe. Pasiwe na kusudi baya au la choyo nyuma yake. Kuna uzalendo wa uwongo vilevile ambao ni hila tufanyayo kwa makusudi yetu wenyewe ya choyo kwa sababu ya nia mbaya za kujitajirisha. Uzalendo wa kweli hutokana na mapenzi yasiyo na choyo ya nchi zetu na heshima yetu ya historia na malezi. Uzalendo usitufanye kujiona kwamba sisi ni watu azizi ulimwenguni na makabila mengine yote si kitu.
Mapenzi ya nchi zetu huonekana kama maono bora lakini hayana maana kama hayachukuani na matendo. Uzalendo wa matendo tu ndio wenye thamani nchini iwapo katika hatari ya shambulio la adui. Mapenzi ya mtu kwa nchi yasiyo ya matendo yanaweza kuwa mema katika nyakati za amani, lakini katika nyakati za vita uzalendo huthibitisha unyofu wake katika kitali. Uzalendo hutaka sadaka za maisha, jamaa, mali na kila kitu cha mtu. Watu wanaotoa sadaka za maisha yao kwa sababu ya nchi zao ni mashahidi.

Maswali
(a) Mwandishi ana misimamo gani kuhusu uzalendo?
(b) Mwandishi anatoa angalizo gani kuhusu uzalendo?
(c) “Kupinga pishi ya hoja zako kwa ukufu wa hoja zao.” Usemi huu una maana gani kulingana na
habari uliyoisoma?
(d) Andika kichwa cha habari kinachofaa kwa kifungu cha habari ulichosoma.


Ufahamu
6

Soma kwa makini kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali yatakayofuata:
Kwa neno zima uzalendo ni mapenzi ya nchi. Mapenzi haya hayafanyiki kwa njia za kubuniwa na watu lakini yamekwishatangulia kuwa katika mioyo yetu. Uzalendo ni tabia ya maumbile, nasi tunayo toka wakati wa kuzaliwa. Tunafikiri habari za nchi yetu kama tufikiriavyo habari za baba na mama zetu; kwa hivi kila mtu anajali sana mahali alipozaliwa.
Baadhi ya watu hawakubali nao wako tayari siku zote kupinga pishi ya hoja zako kwa ukufi wa hoja zao. Wao hufikiri kwamba uzalendo ni maono ya ushupavu na dalili ya uchache wa ustaarabu wa moyo. Kwao uzalendo ni imani ya kishenzi, kwa sababu hutenga kando nchi nyingine.
Wanadai kwamba mtu ni lazima apende ulimwengu mzima na watu wa ulimwengu hufanya kila mtu kuwa raia wa dunia si wa mahali pake padogo pajulikanapo kama nchi yake. Lazima niseme kweli kwamba wazo la udugu wa ulimwengu ni bora kwa makisio lakini kwa matumizi haliwezekani. Bora katika watu ni yule apendaye nchi yake kwanza. Kuna mashaka makubwa kama mtu anaweza kuamini katika mapenzi ya udugu wa ulimwengu bila kupenda nchi yake ikiwa hivyo, uzalendo huthibitisha ubora wa kupenda sehemu ya ulimwengu ambayo ndani yake tumezaliwa.
Mapenzi ya mtu kwa nchi yake hayaoneshi chuki ya nchi nyingine za ulimwengu. Uzalendo wa uwongo ndiyo utufanyao kuchukia nchi nyingine. Aidha, lazima tupende nchi zetu kwa sababu ya nchi zenyewe. Pasiwe na kusudi baya au la choyo nyuma yake. Kuna uzalendo wa uwongo vilevile ambao ni hila tufanyayo kwa makusudi yetu wenyewe ya choyo kwa sababu ya nia mbaya za kujitajirisha. Uzalendo wa kweli hutokana na mapenzi yasiyo na choyo ya nchi zetu na heshima yetu ya historia na malezi. Uzalendo usitufanye kujiona kwamba sisi ni watu azizi ulimwenguni na makabila mengine yote si kitu.
Mapenzi ya nchi zetu huonekana kama maono bora lakini hayana maana kama hayachukuani na matendo. Uzalendo wa matendo tu ndio wenye thamani nchini iwapo katika hatari ya shambulio la adui. Mapenzi ya mtu kwa nchi yasiyo ya matendo yanaweza kuwa mema katika nyakati za amani, lakini katika nyakati za vita uzalendo huthibitisha unyofu wake katika kitali. Uzalendo hutaka sadaka za maisha, jamaa, mali na kila kitu cha mtu. Watu wanaotoa sadaka za maisha yao kwa sababu ya nchi zao ni mashahidi.

Swali:

Andika muhtasari wa aya mbili (2) za mwisho za habari uliyoisoma kwa maneno yasiyozidi sitini
(60).


Ufahamu
7

Soma kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali yatakayofuata:
Sikukuu ya kusherehekea uvunaji wa viazi vipya ilikuwa inakaribia na Umuofia ilikuwa katika hali ya matayarisho. Hii ilikuwa ndiyo siku ambayo watu walitoa kafara kwa Ani, Mungu wa rutuba ya ardhi na mwamuzi wa mwenendo na uadilifu wa watu wote. Alikuwa Mungu aliyehusika sana na maisha ya watu na mababu wa Umuofia waliozikwa katika ardhi yake.
Kwa sababu hii, sikukuu ilifanywa kila mwaka kabla mavuno hayajaanza. Hakuna mtu ambaye angeweza kula viazi vipya kabla havijatolewa sadaka kwa Ani au Mahoka wa mababu wa Umuofia. Watu wote waliifurahia siku hii na kuingoja kwa u chu mkubwa kwa sababu yalikaribia majira ya vyakula maridhawa mwaka mpya. Watu wote waliokuwa na viazi vya mwaka uliopita ilibidi wavitupilie mbali kabla ya sikukuu hii haijaanza. Mwaka mpya ulitakiwa kuanzwa na vyakula vipya vilivyo vinono. Haikuwa heshima wala jambo la faraja kuendelea na vile vilivyokauka kutoka mwaka jana. Hata vyombo vya kupikia na vya kulia vilioshwa barabara. Kinu kile ambamo viazi vipya vilitwangwa kililazimu kusuguliwa sana.
Sikukuu ya viazi lilikuwa tukio la nderemo Umuofia nzima. Yeyote aliyekuwa na m kono wenye nguvu kama wazee wasemavyo alitegemea kualika wageni wengi kutoka karibu na mbali. Okonkwo aliwaalika ndugu wa wake zake na kwa sababu alikuwa na wake watatu, wageni hao walikuwa wengi wa kutosha.
Lakini ingawa hivyo, Okonkwo hakuwa mtu wa kufurahia sikukuu za aina yoyote. Ni kweli kwamba yeye aliweza kula sana, hata alipokunywa tembo alimaliza vibuyu vikubwa lakini kule kukaa bure bila kazi ndiko kulikomfanya asiwe na furaha. Furaha yake ilikuwa katika kazi ya shamba.
Sasa sikukuu ilikuwa imekaribia na wake zake Okonkwo walisugua kuta za vibanda vyao kwa udongo wa aina mbalimbali. Wao wenyewe walijipamba kwa kuchorachora matumbo yao na migongo. Wageni wengi walikuwa wamealikwa hata Ikemefuna alikuwa katika s hamrashamra hiyo. Kwao pia kulikuwa na sikukuu kama hii lakini hapa ilionekana kubwa na ya kufana zaidi. Na kwao sasa kilikuwa kitu kilichoanza kupotea katika dunia ya kumbukumbu yake.

Maswali
(a) Eleza sababu mbili (2) zilizowafanya wananchi wa Umuofia waisubiri kwa uchu mkubwa siku iliyoelezewa kwenye kifungu cha habari.
(b) Kwa mujibu wa kifungu cha habari, eleza sifa moja (1) iliyomtofautisha Okonkwo na watu wengine wa Umuofia.
(c) Eleza maana ya maneno au kifungu cha maneno kilichokolezwa wino.
(d) Unafikiri ni sababu ipi kubwa iliyosababisha kutupwa kwa viazi vyote vya zamani na vyombo vyote kuoshwa?
(e) Andika kichwa cha habari kisichozidi maneno matano (5) kinachofaa kwa habari uliyosoma.


Ufahamu
8

Soma kifungu cha habari kifuatacho kisha andika ufupisho wa maneno sitini (60) kuhusu habari hiyo. Kwa miaka mingi baadhi ya mila na desturi zetu zimetufunga hadi kutufikisha mahali ambapo imekuwa ni vigumu kwetu kubaini ukweli kuhusu mambo muhimu yanayotuzunguka, yakiwa ni yale yanayohusu sisi na miili yetu na yale yaliyonje ya miili hii. Kwa mfamo hadi leo kuna watoto wa umri mkubwa kufikia miaka saba ambao hawajui majina ya baba au mama zao. Lakini pia kuna vijana wa umri wa kuvunja ungo au balehe ambao hawajui ni kwa vipi mtoto anapatikana hasa maeneo ya vijijini. Kuna watu wazima ambao hadi leo mjadala kuhusu kifo ukiingizwa kenye mazungumzo huwa hawako tayari kusikiliza wakiamini kuwa huo ni mwiko na uchoro mkubwa. Hali hii kwa sehemu kubwa inatokana na desturi na mila zetu ambazo zimepogoka na zinahitaji kutazamwa upya kama zina faida kwa jamii. Baadhi ya mambo ambayo yamekuwa yakichukuliwa kama mwiko mkubwa kuyajadili hadharani au hata kati ya watu zaidi ya mmoja ni yale yanayohusu mbegu za kiume, yai la mwanamke na upatikanaji wa mimba.
Siyo jambo la siri kwamba mada zenye kuhusu mambo haya ni nadra sana kujadiliwa katika jamii zetu na wengi ni maamuma kabisa kuhusiana na masuala haya. Inawezekana ikawashangaza wengi pale mtu atakaposema kuwa mwanamume anaweza kumpa mimba mwanamke bila mwanamume huyo kukutana kimwili na mwanamke anayehusika.


Ufahamu
9

Soma kwa makini kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali yanayofuata:
Misitu ya nchi ni mingi sana hata wakati mwingine tunadanganyika kuwa haitakwisha kamwe.

Tunaamini kwamba tunaweza kuendelea kuitumia miti yake na kuikata kwa ajili ya kupata mashamba na malisho ya wanyama wetu bila kujishughulisha kupanda au kuhifadhi mingine kwa ajili ya siku za mbele. Fikiria tulivyo na mawazo potofu. Fikira mbaya kama hizo wanazo watu wengi nchini mwetu. Kwa hiyo imenilazimu kuwaonesheni kuwa misitu ni lazima ilindwe na haitalindwa kwa manufaa ya kizazi chetu cha sasa tu, bali pia kwa ajili ya vizazi vyetu vijavyo.
Basi mjue kuwa kama misitu yote itakatwa patakuwa na upungufu mkubwa wa mbao na pia upungufu wa maji ambao ni mbaya zaidi. Ubaya kama huu hautakiwi utokee katika Taifa letu linalosonga mbele. Hatuwezi kuruhusu uharibifu wa misitu yetu uendelee kufanyika kwa sababu unarudisha nyuma hali ya maisha yetu na unazuia ustawi wa nchi yetu. Hebu fikiria kwanza maisha yetu yatakuwaje iwapo miti itakosekana taabu
ya kupika, gharama ya kujenga kwa chuma, mawe au udongo ulaya badala ya miti. Gharama ya viti, vitanda na meza ikiwa vitatengenezwa kwa chuma tu. Halafu fikiria kama maji yote yakikauka, ninyi nyote mwajua shida zitakazotokea, kwa hiyo hatutaki kabisa shida kutokea.
Kwa nini tuwe na shida ya kukosa maji katika sehemu ambazo zina maji ya kutosha? Basi inatupasa kuona kwamba kuna ulazima wa kuhifadhi misitu kwa ajili ya matumizi ya leo na kesho. Bila shaka sasa utajiuliza mwenyewe. Je, siwezi kukata kabisa misitu ili niweze kulima? Jibu ni kwamba unaweza kabisa, lakini ni katika sehemu zile ambazo hazikuhifadhiwa. Tena ifahamike kwamba sehemu ambazo zimehifadhiwa ni chache sana ukilinganisha na mapori makubwa yaliyobaki wazi kwa ajili ya kilimo.
Sasa nataka kusisitiza hasa juu ya misitu iliyohifadhiwa. Hizi ndizo sehemu za misitu ambazo ni za lazima sana, na inatakiwa zihifadhiwe daima kwa matumizi ya faida ya Taifa. Misitu iliyohifadhiwa ni misitu inayotazamiwa kudumu daima nchini. Inatunzwa ili itumiwe kwa utaratibu ulio bora kwa kizazi hata kizazi. Kwa wakati ujao misitu hiyo itatoa mbao za kujenga nyumba, shule, hospitali na majengo mengine, pia kutengeneza viti, meza, makabati, milango, madirisha na masanduku. Hata sasa, mbao nyingi zitumikazo hutokana na miti iliyoota katika misitu iliyohifadhiwa. Lakini kwa sababu ardhi yenye misitu ya aina hiyo inahitajiwa sana kwa kilimo, itatubidi kuanza kuotesha misitu mipya kwa ajili ya mahitaji yetu. Basi ni lazima niwakumbushe wananchi kuwa miti iliyomo katika misitu iliyohifadhiwa haitatosha kufanyia kazi zetu zote ili kuinua maisha ya watu na kuinua
uchumi wa nchi. Misitu iliyohifadhiwa lazima iongezwe kwa kupanda miti mingine, kwa mfano hivi sasa Idara ya misitu inapanda miti kati ya eka elfu nne na tano kila mwaka na pia inaangalia miti ya asili katika sehemu kubwa kabisa ya nchi hii.

Maswali
(a) Kwa mujibu wa habari uliyosoma watu wengi hufikiria nini juu ya misitu?
(b) Mwandishi wa habari hii anasema ni jambo gani huleta uharibifu wa misitu?
(c) Mwandishi anashauri misitu ikatwe katika sehemu gani?
(d) Je, ni madhara gani yatatokea endapo misitu itatoweka kabisa?
(e) Je, ni sahihi kusema kuwa kwa vile kuna misitu iliyohifadhiwa hakuna haja ya kushughulika na kupanda miti nchini? Kwa nini?


Ufahamu
10

Soma kwa makini kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali yanayofuata:
Misitu ya nchi ni mingi sana hata wakati mwingine tunadanganyika kuwa haitakwisha kamwe.

Tunaamini kwamba tunaweza kuendelea kuitumia miti yake na kuikata kwa ajili ya kupata mashamba na malisho ya wanyama wetu bila kujishughulisha kupanda au kuhifadhi mingine kwa ajili ya siku za mbele. Fikiria tulivyo na mawazo potofu. Fikira mbaya kama hizo wanazo watu wengi nchini mwetu. Kwa hiyo imenilazimu kuwaonesheni kuwa misitu ni lazima ilindwe na haitalindwa kwa manufaa ya kizazi chetu cha sasa tu, bali pia kwa ajili ya vizazi vyetu vijavyo.
Basi mjue kuwa kama misitu yote itakatwa patakuwa na upungufu mkubwa wa mbao na pia upungufu wa maji ambao ni mbaya zaidi. Ubaya kama huu hautakiwi utokee katika Taifa letu linalosonga mbele. Hatuwezi kuruhusu uharibifu wa misitu yetu uendelee kufanyika kwa sababu unarudisha nyuma hali ya maisha yetu na unazuia ustawi wa nchi yetu. Hebu fikiria kwanza maisha yetu yatakuwaje iwapo miti itakosekana taabu
ya kupika, gharama ya kujenga kwa chuma, mawe au udongo ulaya badala ya miti. Gharama ya viti, vitanda na meza ikiwa vitatengenezwa kwa chuma tu. Halafu fikiria kama maji yote yakikauka, ninyi nyote mwajua shida zitakazotokea, kwa hiyo hatutaki kabisa shida kutokea.
Kwa nini tuwe na shida ya kukosa maji katika sehemu ambazo zina maji ya kutosha? Basi inatupasa kuona kwamba kuna ulazima wa kuhifadhi misitu kwa ajili ya matumizi ya leo na kesho. Bila shaka sasa utajiuliza mwenyewe. Je, siwezi kukata kabisa misitu ili niweze kulima? Jibu ni kwamba unaweza kabisa, lakini ni katika sehemu zile ambazo hazikuhifadhiwa. Tena ifahamike kwamba sehemu ambazo zimehifadhiwa ni chache sana ukilinganisha na mapori makubwa yaliyobaki wazi kwa ajili ya kilimo.
Sasa nataka kusisitiza hasa juu ya misitu iliyohifadhiwa. Hizi ndizo sehemu za misitu ambazo ni za lazima sana, na inatakiwa zihifadhiwe daima kwa matumizi ya faida ya Taifa. Misitu iliyohifadhiwa ni misitu inayotazamiwa kudumu daima nchini. Inatunzwa ili itumiwe kwa utaratibu ulio bora kwa kizazi hata kizazi. Kwa wakati ujao misitu hiyo itatoa mbao za kujenga nyumba, shule, hospitali na majengo mengine, pia kutengeneza viti, meza, makabati, milango, madirisha na masanduku. Hata sasa, mbao nyingi zitumikazo hutokana na miti iliyoota katika misitu iliyohifadhiwa. Lakini kwa sababu ardhi yenye misitu ya aina hiyo inahitajiwa sana kwa kilimo, itatubidi kuanza kuotesha misitu mipya kwa ajili ya mahitaji yetu. Basi ni lazima niwakumbushe wananchi kuwa miti iliyomo katika misitu iliyohifadhiwa haitatosha kufanyia kazi zetu zote ili kuinua maisha ya watu na kuinua
uchumi wa nchi. Misitu iliyohifadhiwa lazima iongezwe kwa kupanda miti mingine, kwa mfano hivi sasa Idara ya misitu inapanda miti kati ya eka elfu nne na tano kila mwaka na pia inaangalia miti ya asili katika sehemu kubwa kabisa ya nchi hii.

Swali:

Fupisha aya tatu (3) za mwisho za habari uliyosoma kwa maneno themanini (80).


Ufahamu