Primary and secondary education past papers.
STANDARD 7-SCIENCE-2018-NATIONAL EXAM-TANZANIA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI
05 SAYANSI
Muda : Saa 1:30 Alhamisi, 06 Septemba 2018 asubuhi
Maelekezo
- Karatasi hii ina sehemu A na B zenye jumla ya maswali arobaini na tano (45).
- Jibu maswali yote katika kila sehemu.
- Soma maelekezo yote yaliyoko katika fomu maalum ya kujibia (OMR).
- Jaza taarifa zote zinazohitajika katika fomu ya OMr na katika kurasa zenye swali la 41- 45 kwenye karatasi ya maswali.
- Weka kivuli katika kila tarakimu ya namba yako ya mtihani kwenye nafasi husika katika fomu ya OMR.
- Weka kivuli kwenye herufi ya jibu sahihi kwa swali la 1 -40 kwa mfano, kama jibu sahihi ni A weka kivuli kama ifuatavyo :
- Ukigundua kuwa herufi uliyoweka kivuli si jibu sahihi, futa kivuli hicho kwa umakini kwa kutumia kifutio safi kabla ya kuweka kivuli katika herufi mpya.
- Tumia penseli ya HB kwa swali la 1 hadi la 40; na kalamu ya wino wa bluu au mweusi kwa swali la 41 hadi la 45.
- Simu za mkononi , vikokotozi na vitu vyote visivyoruhusiwa havitakiwi ndani ya chumba cha mthihani.
SEHEMU A(Alama 40)
Katika swali la 1- 40, chagua jibu sahihikisha weka kivuli katika herufi ya jibu hilo katika fomu ya kujibia uliyopewa. Tumia penseli ya HB.
- Ipi jozi sahihi kati ya zifuatazo inahusu sehemu za uzazi katika mimea na wanyama?
- Chavua katika mimea na manii katika wanyama
- Filamenti katika mimea na fallopiani katika wanyama
- Tunda katika mimea na korodani katika wanyama
- Maua katika mimea na uterasi katika wanyama
- Mbegu katika mimea na ovari katika wanyama.
- Ili mimea iweze kuendelea kuishi katika mazingira yake inahitaji
- hewa na uongo
- hewa na maji
- udongo na mbolea
- udongo na maji
- jotoridi na hewa
- Mpunga huzaliana kwa kutumia
- majani
- mbegu
- miziz
- mashina
- matawi
- Kundi linwakilisha wanyama wenye uti wa mgongo?
- Nyoka, ng`e, buibui na mamba
- Konokono, nyoka, kenge na samaki.
- Kenge, nyoka, buibui na samaki.
- Konokono, samaki, chura na mamba
- Mjusi, nyoka, kenge na mamba.
- Kiwavi ni hatua mojawapo ya ukuaji wa
- nyuki
- mbung`o
- funza
- mende
- kipepeo
- Zipi kati ya zifuatazo ni sifa za viumbe hai?
- kukua, kupumua, kusanisi chakula, kujongea
- kukua, kupumua, kulala, kujongea
- kukua, kupumua, kujongea na kuzaliana
- kukua, kuona, kujongea na kuzaliana
- kukua, kusanisi chakula, kujongea na kuzaliana.
- Umeme unasababishwa na mtiririko wa
- electroni
- protoni
- nyutroni
- chaji
- atomi
- Ipi kati ya zifuatazo ni sifa ya kinyonga?
- hubadili mlio wa sauti yake
- huchagua aina ya chakula
- hubadili rangi ya mwili
- hatoi taka mwili
- hubadili mwendo.
- Yupi kati ya wafuatao ni mamalia?
- Konokono
- Bata
- Popo
- Mjusi
- Chura
- Ipi kati ya zifuatazo siyo kazi ya mizizi katika mimea?
- kusharabu madini ya chumvi
- kusharabu maji
- kushikilia mimea
- kutengeneza chakula cha mmea
- kutunza chakula cha mmea.
- Gesi ipi hupunguzwa angani na mimea?
- Kabondayoksaidi
- Oksjeni
- Haidrojeni
- Kabonimonoksaidi
- Naitrojeni
- Ili maji yawe salama kwa kunywa yanapaswa kufanywa nini?
- Kuchemshwa na kufunikwa
- Kuchujwa na kuhifadhiwa
- Kuchemshwa, kuchujwa na kuhifadhiwa
- Kuwekwa juani kutwa nzima na kupozwa
- Kuwekwa kwenye mtungi na kufunikwa
- Yafuatayo ni mahitaji muhimu kwa uhai na ukuaji wa mimea isipokuwa
- mbolea za viwandani
- maji
- hewa ya kabondayoksaidi
- mwanga wa jua
- Udongo wenye rutuba
- Hewa inayohitajika na wanyama ili waishi ni
- Oksijeni
- Kabondayoksaidi
- Naitrojeni
- Haidrojeni
- Kabonimonoksaidi
- Mtu anayekula vyakula vyenye mafuta kwa wingi anaweza kupata
- beriberi
- kifafa
- shinikizo la juu la damu
- kisukari
- shinikizo la chini la damu
- Ugonjwa unaosababishwa na hitilafu katika chembe hai nyekundu za damu huitwa
- Beriberi
- Selimundu
- Saratani
- Kisukari
- Kifuakikuu
- Ni gesi ipi hupungua katika chumba kilichofungwa madirisha wakati kina moto wa mkaa?
- Haidrojeni
- Kabonimonoksaidi
- Kabonidayoksaidi
- Oksijeni
- Naitrojeni
- Nikitu gani tunaweza kutumia ili taswira zetu zionekane vizuri?
- Kioo mbinuko
- Kioo mbonyeo
- Kioo bapa
- Lenzi mbinuko
- Lenzi mbonyeo
- Kwanini ni muhimu kuosha matunda kabla ya kula?
- kuondoa sumu
- kuondoa vimelea
- kuondoautomvu
- kuondoa harufu mbaya
- kuondoa chumvichumvi
- Sehemu ipi ya mfumo wa umeng`enyaji chakula inahusika na umeng`enyaji wa protini?
- Mdomo
- Utumbo mwembamba
- Utumbo mpana
- Umio
- Tumbo
- Magonjwa gani husababishwa na utapiamlo?
- Unyafuzi, kwashako, matege, rovu
- Kiribatumbo, kisukari, kikohozi, kuharisha.
- Unyafuzi, kwashakoo, kupooza, homa ya manjano
- Matege, trkoma, rovu, unyafuzi.
- Kichocho, malaria, kufua kikuu , matege.
- Ni kitu gani hupotea kwa wingi mtu anapoharisha?
- Hewa
- Maji
- Protini
- Wanga
- Vitamini.
- Vipi kati ya virutubisho vinafaa zaidi kwa mtoto mwenye umri chini ya miaka mitano?
- Wanga, maji na protini.
- Protini, vitamini na chumvichumvi
- Chumvichumvi, protini na maji
- Vitamini, wanga na maji
- Kabohaidreti, maji na chumvichumvi.
- Ugonjwa upi kati ya magonjwa yafuatayo husababishwa na bakteria?
- Moyo
- Kifua kikuu
- UKIMWI
- Kichocho
- Kisukari
- Vitu gani kati ya vifuatavyo hupatikana kwenye gari la zima moto?
- Tanki la mafuta, gesi ya kabondayoksaidi na maji
- Tanki la maji , gesi ya kabondayoksaidi na gesi ya oksijeni
- Kikosi cha zimamoto, maji na gesi ya kabondayoksaidi
- Tanki la maji, tanki la gesi ya ukaa na gesi ya asetilini
- Tanki la maji, tanki la gesi mchanganyiko na makoti makubwa.
- Ipi kati ya sentensi zifuatazo inatoa maana ya huduma ya kwanza?
- Msaada wa haraka anaopewa mtu kabla ya kwenda hospitali
- Msaada wa haraka anaopewa mtu baada ya kufika hospitali
- Msaada wa haraka unaotolewa kwa mtu na mtaalamu wa afya
- Msaada unaotolewa kwa mtu aliyezirai.
- Msaada unaotolewa kwa mtu aliyeumwa na nyoka.
- Je, nini utakachokifanya ikiwa utaona nguo alizovaa rafiki yako zinungua kwa moto?
- Kumpaka mafuta
- Kumweka maji kwenye jeraha
- Kumfunika kwa blanketi au nguo nzito
- Kumpulizia jewa ya oksijeni
- Kumvua nguo ziliokwisha ungua
- Zipi kati ya tabia zifuatazo hazichangii kuenea kwa VVU?
- Ngono, ulevi, kunyonyesha mtoto
- Kuchangia sindano, kuweka damu yenye VVU.
- Kushikana mikono, kucheza, kula pamoja
- Elimu duni kuhusu UKIMWI na ngono zembe.
- Uashratina matumizi ya madawa ya kulevya.
- Ni kwanini watu wanaoishi na VVU wanahitaji vyakula vyenye virutubisho zaidi?
- Ugonjwa wao ni wa muda mrefu
- Maisha yao ni mafupi, hivyo wanahitaji chakula cha kutosha
- Wanapata njaa kila wakati
- Wanahitaji kuimarisha kinga ya mwili
- Wanahitaji kunenepa ili kuepuka unyanyapaa.
- Njia sahihi ya kumtambua mtu mwenye virusi vya UKIMWI ni
- kupima kifuakikuu
- kupima mwenendo wa joto la mwili
- kuangaliakama amekonda kwa muda mfupi
- kuangalia kama ana vidonda mdomoni na usoni
- kupima kiwango cha kinga kwenye damu.
- Ni kitendo kipi kinaonesha kuwa hewa huchukua nafasi?
- Kupumua kupitia mdomoni na puani.
- Mapovu ya hewa kutokea chupa ya maji inapozamishwa ndani ya maji.
- Kupiga chafya na kukohoa kwa muda mrefu.
- Mvuke unapopita hewani.
- Kutumbukiza jiwe ndani ya kopo chirizi na maji kumwagika.
- Chunguza kielelezo Namba 1 kisha jibu swali linalofuata:
Kipi kati ya vifuatavyo kinaonesha tabia ya mwale wa mwanga unapopenya kwenye maji?
- II
- IV
- III
- I
- IV
- Nini kitatokea endapo bilauri iliyojazwa maji na kufunikwa kwa mfuniko wa kioo itageuzwa juu chini?
- Maji yatamwagika
- Mfuniko utatoka
- Bilauri itapasuka
- Maji hayatamwagika
- Maji yatachuruzika
- Ni hatua gani muhimu hufuata baada ya kubaini tatizo katika jamii?
- Kuanza uchunguzi wa kina
- Kubuni dhanio
- Kuandaa dodoso
- Kuandaa majaribio ya kisayansi
- Kukusanya taarifa na data.
- Upi ni mpangilio sahihi wa kuandika ripoti ya jaribio la kisayansi?
- Lengo, njia, vifaa, matokeo, hitimisho
- Vifa, lengo, njia, matokeo, hitimisho
- Njia, lengo, vifaa, hitimisho, matokeo
- Njia , lengo, hitimisho, matokeo, vifaa
- Lengo, vifaa, njia, matokeo, hitimisho.
- Ni kwa namna gani chuma huzuiwa kisipate kutu?
- Kwa kukipaka majivu
- Kwa kukiosha na maji
- Kwa kukipaka rangi
- Kwa kukifunika kwa udongo
- Kwa kukifunika kwa masizi
- Ipi kati ya orodha zifuatazo ni kundi la metali?
- Klorini, zinki, almasi na dhahabu
- Chuma, kaboni, naitrojeni na oksijeni
- Oksijeni, zinki, salfa na klorini
- kopa, chuma, kabonmonoksaidi na zinki
- Dhahabu, zinki, aluminiam na silva
- Mfano mmojawapo wa elementi ni
- maji
- Chumvi
- hydrojeni
- Sukari
- Kabondayoksaidi
- Mawingu yanaposhuka na kukaribia uso wa dunia huitwa
- Ukungu
- Umande
- Mvuke
- Barafu
- Mvua
- Chunguza kielelezo Namba 2, kisha jibu swali linalofuata:
Herufi P inawakilisha
- Mwale mtuo
- Mwale akisi
- Mwale pindu
- Mwale sambamba
- Mwale mkabala
SEHEMU B ( Alama 10)
Katika swali la 41-45, jibu kila swali kwa kuandika majibu katika nafasi wazi uliyopewa. Tumia kalamu ya wino wa bluu au mweusi.
- Kielelezo Na. 3 kinaonesha idadi ya wagonjwa waliopokelewa katika hospitali ya Mlingotini mwaka 2017 kutibiwa.
Kokotoa asilimia ya wagonjwa waliokuwa na magonjwa yasiyo ya kuambukizwa.
- (a) Orodhesha mahitaji mawili muhimu kwa utoaji wa mbegu ya mmea.
(b) Mapacha wasiofanana wanatokana na nini?
- Bainisha njia mbili zinazoweza kutumiwa katika kuwasilisha data za uchunguzi zilizochambuliwa.
- Onesha kwa kila mchakato kuwa ni badiliko la kiumbo au badiliko la kikemikali:
(a) Maji kuwa mvuke
(b) Karatasi kuungua
(c ) Chuma kupata kutu
(d) Kuganda kwa soda
- Ikiwa mwanafunzi atanyanyua mzigo kwa kani ya nyutoni 10 na kuupeleka nyumbani umbali wa meta 500;je atafanya kazi kiasi gani? (Tumia nafasi wazi uliyopewa kuonesha njia na jibu).
News & Updates | Recently
Recent Updates |
---|
2024-10-07: questionsQuestions Uploaded on 2024-10-07 |
2024-05-02: questionsQuestions Uploaded on 2024-05-02 |
2024-03-29: questionsQuestions Uploaded on 2024-03-29 |